Vitabu vya Dini husema mwenye nacho huongezewa na asiyekuwa nacho hata kile kidogo alichokuwa nacho hunyan’ganywa Si ndio?sasa kuna Muda Dunia hufanya Virse versa, kuna Muda dunia humshusha yule anayestahili kupandishwa na anayestahili kushushwa humpandisha zaidi, yaani vurugu kweli kweli mpaka unajiuliza kwani ni nini? Dunia, unamaliza hapo unajiuliza kuna uhusiano gani? kati ya ubonge na udalali kazi ngumu na sigara, boda boda na maneno mengi, ufupi na ubishi ama urefu na uzembe? hahahaha! apa ndio ujiulize kati ya mamba na kiboko nani kiboko? Ashante Shana hii ni supa12 subscribe twende sawa
Unamfahamu Rodrygo Silva de Goes, mwamba mwenye uwezo wa maajabu, lakini chaajabu Dunia ya soka inajifanya kama haioni uwezo wake, imeamua ifunike kombe mwanetu apite.
Daaah inasikitisha sana, Rodrygo ni moja ya wachezaji wenye uwezo mkubwa kiwanjani, na anajua kulitendea haki boli sio tu brazil bali hata pale santiago bernabeu wanaujua moto wake, ni kijana mwenye rekodi nyingi za kuvutia lakini huwezi amini hazijawahi kuwavutia hata waandaaji wa ballon d’or,
Karibu katika makala safi ya mwanasoka wa kibrazil anayekipiga Real Madrid, Rodrigo, hapa utaweza kumfahamu kiundani tutaangazia maisha yake ndani na nje ya soka.
kabla hatujaendelea, kama bado hujasubscribe channel yetu hii ya dino television fanya kusubscribe muda huu ili uwe wa kwanza kupata updates zote kutoka kwetu,
Jion ya jumanne ya tarehe 9, january mwaka
2001, Katika mji wa Osasco kusini mashariki mwa sao pauli, Brazil, katika familia ya mzee Eric Batista De Goes, zilisikika kelele za kichanga akilia, kilio kilicholeta furaha kwa Denise Goes, Denise anauaga ubinti baada ya kuleta kiumbe kipya Duniani naam ni mtoto wa kiume aliyepewa jina la Rodrygo. huenda jioni ile kila mtu alitabiri yake kuhusu Rodrygo, huenda kuna waliotabiri labda atakuwa Daktari? Labda akikuwa atakuwa rubani, Lakini baba yake Eric De Goes alivyomtazama Rodrygo aliiona miguu ya mpira na aliona kipaji kikubwa cha boli ndani yake, kama ilivyokuwa kwake Eric de goes alikuwa mchezaji aliyecheza katika vilabu kadhaa brazil japo hakuwahi kufanikiwa kucheza ligi kuu wala timu ya taifa ya Brazil 🇧🇷 ila anatajwa kuwa moja ya right back mzuri kwa wakati wake.
Rodrygo alilewa katika mazingira ya dini sana, wazazi wake ni waumini wazuri kanisani kwahiyo kanisani yalikuwa makao yake muda mwingi.
Maisha yake ya Soka yalianzia katika akademi ya vijana ya Santos mwaka 2011 akiwa na umri wa miaka kumi tu, mwanzoni rodrigo alianzia katika timu ya futsal. Rodrygo alisafiri nchi nyingi akiwa na Santos, akicheza mchezo wake pendwa wa futsal chini ya kocha mashuhuri wa futsal Barata ambaye pia aliwahi kuwa mwalimu wa Neymar, video iliyopostiwa katika YouTube rodrygo akiwa na City Futsal katika eneo la Dallas huko Texas, Marekani.
Mnamo Julai 21, 2017, Rodrygo alisaini mkataba wake rasmi wa kwanza, akiwa na santos mkataba wa miaka mitano. Mnamo na Novemba 1 mwaka huo, akapandishwa hadi kikosi cha wakubwa.
Novemba 4, 2017 Rodrygo aliichezea mechi yake ya kwanza ya ligi ya Série A akiwa katika kikosi cha kwanza, akiingia kama mchezaji wa akiba wa mwisho kuchukua nafasi ya Bruno Henrique katika ushindi wa nyumbani wa 3-1 dhidi ya Atlético Mineiro.
Januari 25 iliyofuata, alifunga bao lake la kwanza la ushindi, akifunga bao la dakika za mwisho katika ushindi wa ugenini wa 2-1 wa Campeonato Paulista dhidi ya Ponte Preta.
Rodrygo aliichezea Copa Libertadores kwa mara ya kwanza mnamo Machi 1, 2018, akichukua nafasi ya Eduardo Sasha katika kichapo cha 2-0 ugenini dhidi ya Real Garcilaso;
akiwa na umri wa miaka 17 na siku 50, alikua mchezaji mdogo zaidi wa Santos kuonekana katika mashindano hayo. Siku kumi na tano baadaye alifunga bao lake la kwanza katika mashindano hayo, akifunga bao la pili la timu yake kupitia juhudi binafsi katika ushindi wa 3-1 dhidi ya Nacional kwenye Uwanja wa Pacaembu; akiwa na umri wa miaka 17, miezi miwili na siku sita, akawa Mbrazil mdogo zaidi kufunga goli katika mashindano hayo kabla ya rekodi yake kuvunjwa na wachezaji wengine waliohitimu kutoka akademi ya vijana ya Santos, Kaiky na Ângelo.
Rodrygo alifunga bao lake la kwanza katika ligi kuu ya kandanda ya Brazil mnamo Aprili 14, 2018, akifunga bao la mwisho katika ushindi wa nyumbani wa 2-0 dhidi ya Ceará. Mnamo Juni 3, alifunga hat-trick na pia alitoa pasi ya mwisho kwa bao la mwisho katika ushindi wa nyumbani wa 5-2 dhidi ya Vitória
Julai 26, 2018, Rodrygo alibadilisha namba ya jezi yake kutoka 43 hadi 9 (namba ambayo tayari alikuwa ameivaa wakati wa Libertadores). Kwa msimu wa 2019, alibadilisha tena namba, sasa hadi jezi namba 11, ambayo hapo awali ilivaliwa na mchezaji mwenzake aliyehitimu kutoka akademi hio ya vijana, Neymar junior.
Rodrygo alifanikiwa kucheza michezo 80 akiwa na Santos huku akifanikiwa kufunga magoal 17.
Mwaka huo huo 2019 Mascout wa real madrid wakavutiwa na uchezaji wake, Don perez akazama mfukoni na kumnunua Rodrygo kwa Euro Million 45 sawa na shilling bilion 1.3 za kitanzania.
Rodrygo akasainishwa mkataba wa miaka 6 kuitumikia real madrid toka mwaka 2019 mpaka 2025,
Septemba 25, 2019, Rodrygo alicheza kwa mechi yake ya kwanza akiwa na real Madrid na akafanikiwa kufunga bao lake la kwanza la Laliga dhidi ya Osasuna ndani ya dakika moja tu.aliyoingia uwanjani.
Rodrygo Alifunga hat-trick yake ya kwanza, na kutoa pasi ya bao kwa klabu hiyo Novemba 6, akiwa na umri wa miaka 18 na siku 301, dhidi ya Galatasaray katika ushindi wa 6-0 katika msimu wa Ligi ya Mabingwa ya UEFA Cl msimu 2019-20 Akiwa mchezaji wa pili mdogo zaidi kufunga hat-trick katika mashindano hayo, lakini pia akawa ni mchezaji wa kwanza aliyezaliwa katika karne ya 21 kufunga katika mashindano hayo. Katika msimu wake wa kwanza,
Rodrygo aliweza kucheza mechi 19, huku akifunga mabao mawili wakati wa msimu wa ligi, huku Real Madrid ikishinda La Liga satander msimu. Novemba 3, 2020, Rodrygo alifunga bao la ushindi katika ushindi wa 3-2 dhidi ya Inter Milan katika Ligi ya Mabingwa, UEFA Cl msimu wa 2020-21
Aprili 12, 2022, baada ya kuingia kama mchezaji wa akiba katika mchezo wa pili wa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa ya UEFA ya 2021-22 dhidi ya Chelsea, alifunga bao la dakika za jioni na kupeleka mchezo hadi dakika extra-time, ambapo Karim Benzema alifunga bao la ushindi kwa kichwa, na kuifanya Real Madrid kusonga mbele hadi nusu fainali. Aprili 30, Rodrygo akasaidia Real kutwaa taji lao la 35 la La Liga baada ya kufunga mabao mawili katika ushindi wa 4-0 dhidi ya Espanyol kwenye uwanja wa Bernabéu. p
Mei 4, wakiwa nyuma kwa bao 0-1 ( aggregate ikisoma 3-5) katika mchezo wa pili wa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Manchester City, alifunga mabao mawili kati ya dakika ya 90 na 91 na kusawazisha mchezo na kuupeleka hadi dakika za ziada. Benzema alifunga penalti na kushinda mchezo kwa 3-1, na kuiruhusu Real Madrid kusonga mbele hadi fainali dhidi ya Liverpool kwa jumla ya mabao 6-5 na hatimaye wakashinda mashindano hayo.Kufuatia ushindi huo wa kusisimua dhidi ya City na michango mingine ya hivi karibuni ya ushindi wa dakika za mwisho, mchango wa Rodrygo kwa timu ulisifiwa licha ya umri wake mdogo na haraka akageuka kuwa shujaa anayeheshimika sana Madrid.
Mnamo Aprili 18, 2023, alifunga mabao mawili katika ushindi wa ugenini wa 2-0 dhidi ya Chelsea katika mchezo wa pili wa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa ya UEFA ya 2022-23, ambao ulihakikisha timu yake inafuzu kwenda nusu fainali kwa ushindi wa jumla wa 4-0. Mei 6, alifunga mabao mawili kwa Real Madrid katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Osasuna katika fainali ya Copa del Rey ya 2023, na kuwa taji lao la 20 katika mashindano hayo.
Mnamo Novemba 2, 2023, Real Madrid ilitangaza kuufanya mabadiliko ya mkataba wa Rodrygo akasaini mkataba mpya uliongezwa ( Extended contract)ambao utamalizika Juni 30, 2028.
Msimu huu wa 2024-2025 ukawa si msimu mzuri sana kwake alipata majeraha mara kadhaa, lakini pia klabu yake haikuwa na wakati mzuri katika mashindano yote makubwa waliyoshiriki hawakubahatika kubeba makombe
Rodrigo amecheza mechi 42 katika mashindano yote akifanikiwa kufunga magoli 11.
Rodrygo tangu ajiunge na real Madrid amecheza michezo 172 huku akifunga magoli 89 na assist 55.
Rodrigo ana Laliga 2
Uefa champions league 2
Fifa club world cup 1
Amechukua spanish champion cup mara 3
Uefa super cup mara2
fifa intercontinental cup mara 1
spanish super cup mara 3.
tuangazie kwa ufupi kuhusu timu yake ya taifa ya brazil
Rodrygo aliitwa kwa mara ya kwanza katika kikosi cha under 17, machi 30, 2017
akaitwa kwa mara ya kwanza timu ya taifa ya wakubwa Brazil mwezi november 2019, katika Superclásico de las Américas dhidi ya Argentina ya Mess mechi ikipigwa Riyadh, Saudi Arabia. brazil wakipoteza kwa goli 1–0 on15 November.
tangu wakati huo kila iitwapo Timu ya taifa ya brazil jina lake likawa lipo katika list,
kwa mara ya kwanza 2022 akafanikiwa kucheza world cup akiwa na brazil
amecheza copa america 2024. na amefanikiwa kucheza michezo 33 na kufunga goal 7.
Nikurudishe kule mwanzo kwanini? mimi Dennis Dinomineta nabaki kuamini kuwa Rodrygo ni underated player, yaani anavochukuliwa si kama alivyo,
Rodrygo Silva de Goes, ni kijana mwenye kipaji cha ajabu sana, nadhani miaka ijayo ukiwatafuta vijana waliokua na vipaji vya dhahabu kutoka brazil jina la Rodrygo halitawahi kukosa, rodrigo alikuwa na ndoto moja tu tangu utotoni: kuwa nyota wa soka na kushinda mataji makubwa na Real Madrid. Alifanikiwa kufikia ndoto hiyo kwa kasi ya kustaajabisha—akifunga magoli ya kusisimua Ligi ya Mabingwa, akisaidia timu yake kushinda mataji, na kuwa shujaa wa mashindano makubwa kama El Clásico na Copa América.
Lakini, kwa kila goli alilofunga na kila mchezo aliodunda, Rodrygo alibaki kwenye kivuli cha wenzake—haswa VinĂcius JĂşnior na Karim Benzema. Hata na uwezo wake wa kipekee wa kudribo mpira, kufunga, na kupiga pasi sahihi, mara nyingi alipewa nafasi ya kuingia kama mbadala au kucheza kwenye nafasi zisizomfaa.
Wakati wa msimu wa 2022-23, Rodrygo alionyesha uwezo wake wa kutosha: ulikuwa ni moja ya msimu bora sana kwake, akifunga magoli 10 na assist 8 katika michezo yote ya ligi, na takwimu zake zikionyesha kuwa alikuwa miongoni mwa wachezaji bora wa Madrid wenye ubunifu na ufanisi. Lakini, licha ya mafanikio hayo, kocha Carlo Ancelotti alimweka benchi mara kwa mara, sometimes akibanwa na waandishi akimtaja Rodrygo kuwa “injury” hata wakati ambao alikuwa tayari kwa mchezo.
kuna kipindi hadi Mashabiki walilalamikia bwana mdogo kutokupata nafasi
Maana ilifika mahali Vini anacheza vibaya, anapoteza mpira, lakini hafanyiwi sabu afu wakati huo unakuta Rodrygo yuko benchi!
mashabiki wakaanza kushinikiza kuwa *”Yeye ndio sababu real madrid kulishinda UCL! Kwa nini wanamsahau? bwana mdogo
Lakini maoni ya mashabiki hayakutosha. Hata baada ya kuiokoa Madrid dhidi ya Manchester City kwa magoli mawili ya kusisimua Ligi ya Mabingwa, alibaki kuwa “mchezaji asiyepewa ile first priority.
Mwaka huu 2025, kuna uvumi kwamba Rodrygo huenda anaweza kuondoka Madrid kwa sababu ya kukosa nafasi ya kuanza katika michezo mingi,
watu wengi husema kuja kwa nyota kama Mbappé kunaweza kuwa kumechangia Rodrygo kutokupata nafasi na sasa anaonekana kama kivuli kwenye timu siyo mchezaji tegemezi.
Binafsi namuona Rodrygo ni mfano wa kipaji cha dunia kilichozuiwa kuangaza kikamilifu. Ana uwezo wa kuwa kati ya wachezaji bora duniani, lakini mfumo wa timu na uamuzi wa kocha umemfanya abaki kuonekana kama “msaidizi” badala ya nyota. Daah Hadithi yake ni ya kuhuzunisha kwa sababu inaonyesha ni jinsi gani soka mara nyingi si tu kuhusu uwezo bali pia ni bahati. kuna muda unahitaji bahati kushine.
Ukiachana na maisha yake ya soka, katika maisha yake nje ya soka Rodrygo ni kijan mpole anayependwa na watu wengi, mwaka wa jana tafiti za wachokonozi wa mambo mitandaoni walidai Rodrygo ndie mchezaji namba moja real Madrid anayewavutia zaidi watoto wakike pamoja na kupendwa na wadada wengi, lakini tayari Rodrigo ana mchumba aitwae Bruna rotta lakini pia ana watoto wawili mapacha wa kiume RAYAN na RAVY aliowapata mwaka 2022, kwa aliyekuwa mpenzi wake aitwae Pamella Cristina Costa
Mnamo Februari 2024, Rodrygo alishirikiana na Juegaterapia na msanii Titocustoms kuzindua kampeni ya kuchangisha fedha dhidi ya saratani ya utotoni. Mpango huo, ambao ni sehemu ya kampeni ya “Kila kitu kitakuwa sawa”, ulihusisha mnada wa vitu vilivyobinafsishwa—ikiwa ni pamoja na sneakers za Nike, koti, mpira, na picha—ili kusaidia watoto walioathirika. Akizungumzia ushiriki wake, Rodrygo alisema, “Soka ni chombo kinachoturuhusu sio tu kukuza maadili ya michezo, bali pia kutoa fursa kwa watu wale wanaohitaji msaada.”
Baba yake Rodrygo alikuwa tayari ametabiri kwamba angekuwa mchezaji wa mpira kabla hata hajazaliwa. Rodrygo ana dada mdogo mmoja, Ana Julya, aliyezaliwa mwaka 2018.