Kuna matukio Mengi yanayotokea katika mchezo wa soka matukio ambayo, yanaacha kumbukumbu kubwa katika maisha ya watu, zinaweza kuwa kumbukumbu njema ama mbaya? Nadhani siyo kitu kigeni kushuhudia watu wakizimia, wengine wakipoteza hadi maisha yao baada ya masikitiko, ama furaha kuzidi wakati wakiangilia mchezo wa mpira miguu, katika matukio ambayo yanaweza kuwa yanaongoza kwa kuwapa heart attack, pressure na pengine kupelekea vifo kwa watu pindi wakiangalia soka basi, ni mikwaju ya Penalty, hii ndio mida pekee ambayo utawaona wale wenye pressure na roho ndogo wakigeuka nyuma, wengine kutoka kabisa katika eneo wanalotazama mpira ili tu wasishuhudie mikwaju ya penalty.
Leo nimekusogezea Mikwaju Mitano ya Penalty iliyobeba hisia kubwa katika soka, ambayo mimi binafsi nimewahi kuishuhudia, nitaanza na namba 5 mpaka nambari 1.

Penalty ya 5: ni penalty ya Kepa Arrizabalaga:

Watch: Kepa fires penalty over the bar after Chelsea keeper was brought on for Carabao Cup final shootout vs Liverpool | Goal.com
Huyu jamaa alikuwa golikipa wa chelsea na hii penalty ilikua katika mechi ya chelsea vs Liverpool,
Ilikuwa ni fainal ya Carabao Cup kati ya Liverpool vs Chelsea mechi ilipigwa pale Wembley Stadium jijini London, Uingereza, ulikuwa ni usiku wa tarehe 27 mwezi February 2022. hii ndio fainal ya kwanza Carabao Cup Chelsea na Liverpool kukutana na fun fact msimu huo Chelsea na liverpool walikutana katika fainal mbili ndani ya msimu mmoja fainal ya Carabao cup EFL na FA cup na fainal zote zilimalizwa kwa penalty na zote liverpool walishinda,
Sasa katika huu mchezo Full time mechi ilimalizika kwa sare ya bila kufungana hadi kwenye extra time Nil Nil, yaani bila bila, game ikabidi imalizwe kwa mikwaju ya penalty oya zilipigwa penalty 11 katika hii mechi, zote chuma kwa liverpool
Sasa hii ndio ilikuwa penalty ya mwisho ya 11 kwa chelsea apo Golikipa aliyetegemewa sana na kocha Thomas tukel kocha wa chelsea kipindi hiko kuja kufanya save bwana Kepa arrizabalaga anapewa penalty ya mwisho kabisa na anapaisha na kuinyima ubingwa klabu yake ya chelsea, kilichowauma zaidi mashabiki wa chelsea ni kitendo cha kocha Thomas tukel kumfanyia sub Eduardo Mendy golikipa aliyefanya saves kibao ndani ya pitch alafu anakuja kumweka golikipa mwingine ambaye anashindwa kusave ata penalty moja.

Penalty ya Nne: Ni Penalty ya Shomari kapombe beki wa klabu ya simba,

Kapombe ala kiapo Simba | Mwanaspoti

April 9, 2025, Shomari Kapombe anaenda kupiga penalty ya mwisho kabisa ya kuwapeleka simba sc katika nusu fainal ya Caf confederation cup katika mechi dhidi ya Almasry, baada ya simba sc kuchezea kichapo cha goli 2 kwa 0 kule nchini misri mechi ya marudiano ikapigwa Jijini Dar es Salaam Mkapa Stadium nyumbani kwa simba sc, simba wakiondoka na ushindi wa magoli 2 katika 90dk aggregateikisoma 2 kwa 2, wakaenda katika mikwaju ya penalty, Penalty zimeshapigwa tatu kwa pande zote huku camara ameshasave mbili, sasa ikafika zamu ya penalty ya Shomari Kapombe, wakati huo Macho ya mashabiki wa simba sc na watanzania wote kwaajumla yakiwa kwa kwa shomy the way, kapombe anaenda kupiga penalty hio akiwa na kumbukumbu mbaya ya miaka miwili iliyopita kumbukumbu ya kupoteza penalty ya mwisho iliyotakiwa kuwapeleka simba sc katika nusu fainal ya Caf champions league baada ya miaka 30, katika mchezo wa robo fainal dhidi ya wydad Casablanca, ni Penalty iliyojaa pressure kubwa sana si kwa kapombe tu bali hata kwa mashabiki wa klabu ya simba waliosubiri kwa takribani miaka 32 kuishuhudia simba sc ikiingia nusu fainal ya mashindano ya Caf, kwa bahati nzuri kapombe anafanikiwa kuikwamisha kambani penalty ile na Simba sc inafanikiwa kutinga nusu fainal ya Caf confederation cup.

Penalty ya 3: ni Penalty ya Gonzalo Montiel, kwenye mchezo wa fainal ya kombe la Dunia mwaka 2022,

Los momentos previos de Montiel al penalti que hizo Campeón a Argentina - Vamos Mi Sevilla

mchezo ambao uliowakutanisha Argentina 🇦🇷 dhidi ya Ufaransa 🇫🇷, hii ni moja ya fainal ambayo haitawahi kusahaulika katika ulimwengu wa soka, kwanza picha linaanza mpaka dakika ya 78 Argentina wako mbele kwa magoli mawili, ndani ya dakika mbili tu dakika ya 79 na 80 kylian mbappe anabadilisha upepo kwa kusawazisha magoli yote mawili, na kwenda extra time Argentina wanaongeza goli moja Ufaransa wakarudisha klyian mbappe akiondoka na hattrik full time 3 kwa 3, wakaenda katika mikwaju ya penalty, ambapo walianza france mbappe akaweka chuma kambani, messi akaweka france wakakosa 2 argentina wakapata kolomuani akaweka upande wa france ikawa ni 3 kwa 2, hii sasa ndio ilikuwa penalty ya mwisho ambayo ilikuwa inaenda kuamua mikwaju iendelee au Argentina wakabidhiwe kombe, Gonzalo Montiel anaaminiwa na kocha kwenda kuipiga penalty mbele ya maligend penalty iliyobeba matumain mengi kwa Argentina wakiwa na kumbukumbu ya kombe lao la world cup walilolichukua
Miaka 36 iliyopita chini ya armando maradona sasa ni utawala wa Messi, mchezaji mwenye profile ya kawaida mchezaji kutoka pale pale katika ligi ya ndani Argentina akikipiga katika klabu ya River plate, bwana Gonzalo Montiel kwanza mwamba hakuwa miongoni mwa wachezaji walionza katika mechi hio lakini Akafanikiwa kuumaliza mchezo baada ya kuizamisha kambani penalty hio na anaandika historia mpya Kwa Lionel Messi, Di maria, Rodrygo de paul, Lautaro Martinez na wengine wengi. That was Crazy 🤪.

PENALT YA 2. Ni Didier Drogba penalty ya Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (Uefa champions league)

Chelsea beat Bayern Munich in dramatic penalty shoot-out to claim the Champions League final - The Mirror

Ilikuwa Jumamosi ya tarehe 19, May 2012: Chelsea dhidi ya Bayern Munich, kwa mara ya kwanza baada ya miaka 28, bayern munich wanapata faida ya kucheza fainal katika uwanja wao wa nyumbani wa Allianz Arena, mchezo. Uliojaa competition kubwa sana 90 dk zikamalizika kwa sare ya goli 1-1, goli la bayern likifungwa na Tomas, La chelsea likifungwa na Didier Drogba, mechi ikaenda katika Extra time dk drogba anacheza rafu kwenye box lao na kusababisha penalty bayern wakampa jukumu robben, robben anapiga penalty hio Peter Cech akasave, extra time ikamalizika moja kwa moja, wakaenda katika mikwaju ya penalti. Didier Drogba, ambaye alikuwa amefunga bao la kusawazisha la kichwa katika dakika za mwisho za mchezo, huyo huyo Didier Drogba aliyesababisha penalty waliokosa bayern, anafunga penalti ya mwisho na ya ushindi kwa klabu ya chelsea na kwa mara ya kwanza Chelsea wanabeba taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya (uefa championsleague)
Hii ni Penalty ambayo hakuna shabiki wa klabu ya chelsea atawahi kuisahau

Penalty ya kwanza: Ni Penalty ya Asamoah Gyan,

Asamoah Gyan's Penalty Miss 10 Years On😭

aliyekuwa mchezaji wa timu ya taifa ya ghana, kipindi hicho asamoah akiwa ni top top player kwenye taifa la ghana, hii ni moja ya Penalty ambayo hakuna mghana wala mwafrika yeyote mpenda soka anaweza kuisahau, ni Penalty iliyojaa pressure kubwa sana, hii Penalty ilipigwa mwaka 2010 katika kombe la Dunia, kwa mara ya kwanza kabisa bara la africa linapata host wa world cup, pale kwa Madiba Africa ya kusini, na hii ndio ilikuwa mara ya kwanza kwa ghana kufika katika hatua ya robo fainal ya kombe la Dunia, na ndio ilikuwa mara yao ya pili kushiriki world cup baada ya ile ya 2006, hii ilikuwa ni mechi dhidi ya timu ya taifa ya uruguay, kipindi cha kwanza kinatamatika ghana wakiongoza kwa goli 1, kipindi cha pili uruguay wanarudisha goli, 90 dk zinamalizika kwa sare, saa ngapi? wasiende extra time? hao mpaka extra time 120 zikamilike, pira likapigwa mpaka dakika za jioooni kabisa ghana wanapata freekick ama pigo huru karibu kidogo na box la kumi na nane ile freekick inapigwa then jamaa anaiunga kwa kichwa na ishamvuka golikipa alafu golini akiwepo mshambuliaji wa uruguay Luis Suarez, mwamba anaamua kujitwisha majukumu ya goli kipa. na kuudaka mpira, pale pale anakula Umeme, na unatengwa mkwaju wa penalty, Penalty anapewa Asamoah Gyan macho yote ya ghana na africa nzima yanamuangalia asamoah, Waganga, mashehe, wachungaji, makando wa daladala mpaka marais wa africa macho yote kwa Asamoah, Jamaa anaenda kupiga penalt hio, akaipiga kifundi kabisa lakini kwa bahati mbaya anakosa penalty ile, baada ya kugongesha mwamba, daah dk 120 zinatamatika kwa sare. wakaenda kwenye mikwaju ya penalty ghana wakatolewa na Uruguay kwa mikwaju minne kwa miwili. kumbuka kipindi hicho kama Asamoah Gyan angefunga penalty ile Ghana lingekuwa taifa la kwanza kutoka afrika kufika katika hatua ya nusu fainal ya kombe la Dunia,
hii ni Penalty ambayo ilimfanya asamoah Gyan astafu kwa muda kuitumikia timu yake ya taifa, kila kona ya ghana, kila kona ya africa ilimuona kama jamaa kakosa penalty kimakusudi vile, kila mtu alimtupia lawama jamaa, kama maneno yangekuwa sumu basi kipindi kile jamaa tungempoteza duniani 😄

Binafsi kwangu mimi katika maisha yangu ya ufuatiliaji wa kabumbu hii ndio
Mikwaju mitano ya penalti ambayo nimewahi kuishuhudia mikwaju ambayo imeacha alama isiyofutika katika historia ya soka, ikionesha jinsi mchezo huu unavyoweza kuwa na mvuto na msisimko mkubwa, huku ukiwakumbusha wachezaji na mashabiki kuwa chochote kinaweza kutokea hadi filimbi ya mwisho. Je? Ni Penalty gani? Unaikumbuka zaidi kati ya hizi na je? Ni zipi Penalty zako bora za muda wote ulizowahi kuzishuhudia katika maisha yako ya soka? Drop comment yako hapo kwenye comment hii hapa ni supa12 ya dino television subscribe channel yetu ya dino television ili uwe wa kwanza kupata updates zote kutoka kwetu .

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *